Rais Magufuli alisema
:
“Hatuna tena muhali na wahalifu wanaotumia silaha wala kujihusisha na ugaidi, Watanzania walishasahahu kunyang’anywa fedha zao, sasa tunasema mama mkanye mwanao, mke mtunze mumeo, vinginevyo mtawakosa. ”
habarileo Saturday, February 27, 2021 11:12:00 AM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Watendaji wa Serikali wawe wepesi kutoa taarifa sahihi kwa waandishi wa habari, utakuta yamefanyika mambo mazuri lakini hayatolewe na wananchi hawayafahamu, tusiogope kukosolewa, lakini vyombo vya habari toeni taarifa za ukweli bila kuweka chumvi, zingatieni ukweli,”
mtanzania Saturday, February 27, 2021 10:18:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Vyombo vya habari mnajitahidi kutoa habari, lakini mtangulize sana uzalendo na hakikwa yule anayeandikiwa habari, kumekuwepo na uzushi sana mara fulani kafa ni mambo ya ajabu,”
mtanzania Saturday, February 27, 2021 10:18:00 AM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Muheshimiwa IGP umezungumza kuhusu hao wafungwa wa uhalifu mbalimbali wa kutumia silaha ambao wakifungwa wakirudi wanaendelea kurudia matukio hawataki kuyaacha, kama alikuwa jambazi anaendelea na ujambazi muwalazimishe sasa wayaache kwa nguvu na hilo najua halitakushindwa IGP”
habarileo Friday, February 26, 2021 3:47:00 PM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Kutopata mafao ni tatizo la wakubwa wenu wizarani kama mpo hapa wastaafu mumlaumu Waziri mwenye dhamana na watendaji wake huo ndio ukweli wakitaka wastaafu kulipwa watalipwa tena haiwezi kuchukua hata siku tano kama watakuwa na mawasiliano mazuri na Wizara ya Fedha,”
habarileo Friday, February 26, 2021 2:57:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
"Manispaa ya Ilala mnastahili, hamkupendelewa, ni haki yenu kwa sababu hata katika mapato mnaongoza. Kwa nini mlinganishwe na manispaa nyingine, na kwa uamuzi huo aliyekuwa Meya wa Ilala ndiye Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam pamoja na Naibu Meya wake"
habarileo Friday, February 26, 2021 7:01:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
"Nyie ndio mabosi wa jiji hili (Dar es Salaam) na nyie ndio mabosi wangu nitakapokuwa nakuja jijini humo, na madiwani wa Manispaaa ya Ilala ndio madiwani wa jiji na bajeti yenu itaongezeka na kuwa kubwa ili itumike kusaidia kutatua changamoto za jiji na maeneo yake yote,"
habarileo Friday, February 26, 2021 7:01:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Wabunge na watendaji wote lazima tuwe tunatembelea maeneo yetu na sio kusubiri kuona taarifa mitandaoni, kama ile Shule ya King’ongo, tujipange kutatua kero, nashukuru RC (Mkuu wa Mkoa) wa Dar es Salaam alivamia pale na kuanza kushughulikia, lakini kwa kweli ile shule ingekuwa hadi leo haijajengwa mngekoma, nilitaka kutoa demo, nigeanzia na RC, DC (Mkuu wa Wilaya), Mkurugenzi, sijui Mwenyekiti wa council (baraza) mpaka mwenyekiti wa Kijiji na Waziri”
habarileo Thursday, February 25, 2021 9:44:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Tunawajibu wa kuwatumikia wananchi huo ndio mkataba wetu kwao, kwa hiyo RC nakushukuru malaika walikugusa ukawahi haraka haraka, nilikuwa nakuangalia, nikasema una bahati kwa sababu mkuu wako wa wilaya alishaanza kulalamika akasema wanatumiwa, sasa wanatumiwa wakati wanaeleza ukweli, kwa hiyo sisi tunawajibu wa kutekeleza yale tunayotakiwa kutekeleza”
habarileo Thursday, February 25, 2021 9:44:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Tumepata alama ya pekee ya jiji hili, tuitunze idumu miaka mingi, barabara hizi zinasaidia kuondoa msongamano wa magari kwenye makutano haya, kwa maana sasa unapita moja kwa moja kwenda ama Mwenge, au Kimara, au Buguruni au Posta hakuna tena msongamano,”
habarileo Thursday, February 25, 2021 9:44:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Kwa hiyo tujiandae kisaikolojia wale waliokuwa wanautaka umeya wa jiji la Dar, Meya atapatikana kutoka Ilala au mojawapo ya Manispaa za hapa,draft (rasimu) ya kubadilisha jiji hili nimeshaletewa na Jaffo nikitoka hapa nakwenda kuisaini ili turahisishe mambo, tuokoe fedha zilizokuwa zinapotea”
habarileo Thursday, February 25, 2021 9:44:00 AM EAT
Rais Magufuli alisisitiza
:
“Tuendelee ndugu zangu Watanzania kusimama na Mungu, tulishinda mwaka jana, inawezekana hili ni jaribu jingine, nalo tukisimama na Mungu tutashinda, tusitishane na kuogopeshana tutashindwa kufika. Inawezekana kuna mahali tumemkosea Mungu, inawezekana kuna mahali tunapata jaribu kama Waisraeli walivyokuwa wakienda Kaanani. Tusimame na Mungu ndugu zangu Watanzania,”
habarileo Saturday, February 20, 2021 5:04:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Hata sasa hatutaweka ‘lock down’ kwa sababu tunajua Mungu yupo siku zote. Niliona nitoe huu wito ndugu zangu kwa sababu mimi ni kiongozi wenu, nina wajibu wa kuwakumbusha kwamba taifa hili liko mikononi mwa Mungu na Mungu ataendelea kusimama,”
habarileo Saturday, February 20, 2021 5:04:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Kijazi alikuwa hakai ofisini, alikuwa anatembelea barabara zake. Mwaka 2000 baada ya uchaguzi, nikachaguliwa kuwa Waziri, nilipokuwa Waziri nikajua Rais Mkapa ataniletea Katibu Mkuu mwingine, siyo kawaida kwa waziri kuomba Katibu Mkuu, nikaja Ikulu kumuona Mzee Mkapa, kumuomba Balozi Kijazi awe Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi,”
habarileo Saturday, February 20, 2021 5:04:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Ikaisha miaka miwili. Mwaka 2019 sikupata. Nikamwongeza tena miaka mingine miwili, kwa hiyo natoa pole sana kwa familia,”
habarileo Saturday, February 20, 2021 5:04:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Mheshimiwa Maalim Seif Sharif Hamad, aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar. Natoa pole kwa Rais wa Zanzibar Dk Mwinyi, familia, Wazanzibari, wanachama wa ACTWazalendo na Watanzania wote. Mungu amweke mahali pema peponi, Amina,”
habarileo Thursday, February 18, 2021 8:49:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Bidhaa zenu zinaitwa Korie, naomba mwekezaji aangalie kutengeneza jina jingine linalohusu Tanzania kwa sababu Tanzania tunazalisha vitu vingi, kwa mfano maparachichi yanazalishwa Iringa yanawekwa nembo ya nchi zingine, inafaa pawepo na jina linalotangaza Tanzania kwa kuwa itakuwa njia ya kuitangaza nchi yetu. Tuwe na nembo ya Kitanzania ambalo ni jambo muhimu katika kujenga uzalendo, lazima tujivunie uzalendo wetu,”
habarileo Saturday, February 13, 2021 6:18:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Nampongeza mwekezaji kwa kujenga kiwanda hiki kwa kwa gharama ya Dola za Marekani milioni 20 sawa na zaidi ya Sh bilioni 40. Kiwanda hiki ni kikubwa kuliko vyote nchini na kina uwezo wa kukoboa tani 288 za mpunga kwa siku, kinatoa ajira ya watu 75 za moja kwa moja lakini wanufaika ni wengi,”
habarileo Saturday, February 13, 2021 6:18:00 AM EAT
Rais Magufuli alisisitiza
:
“Wote waliopewa viwanda na hawajaviendeleza tuvichukue, waziri usichelewe wala kutazama sura ya mtu, tena wakati huu ambao mimi nipo ndiyo wa kuyang’anya viwanda hivyo, nikiondoka yatarudi yaleyale,”
habarileo Saturday, February 13, 2021 5:29:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Ndiyo maana leo (jana) nakupongeza sana Rostam kwa uwekezaji huu, kweli nakupongeza kwa sababu ndugu yako Abood mbunge wa hapa ameshindwa kuviendesha viwanda viwili vya Canvas na Moproco. Kiwanda cha Moproco kilikuwa kinazalisha mafuta ya kupikia, lakini mbunge wetu ulipewa hivi viwanda tangu mwaka 1996 mpaka uliponyang’anywa mwaka jana, kwa hiyo ukawanyima ajira wapiga kura wako,”
habarileo Saturday, February 13, 2021 5:29:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Sasa nimeshangaa sana na kweli nimeumia sana, mtu anakuja na kiroba chake cha vitunguu, akifika hapa anamkuta mtu wa manispaa anataka kudai pesa ya kuingiza biashara, anadai pesa ya kizimba na zingine, lakini kitu kingine nilichokiona humu kuna watu waliopewa vizimba vyao bila tatizo, lakini wapo wengine waliopewa vizimba kwa kukodishwa na madalali,”
habarileo Friday, February 12, 2021 4:08:00 AM EAT
Rais Magufuli alisisitiza
(
about Rais Magufuli
)
:
“Sitaki raia wasumbuliwe wakati mimi nikiwa Rais,”
habarileo Friday, February 12, 2021 4:08:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Mheshimiwa Jaji Mkuu Watanzania watakuheshimu kwa historia. Umefanya mambo mengi lakini hili nalo limalizie. Mheshimiwa Jaji Kiongozi na waheshimiwa majaji, ndugu zangu wananchi wanalia kwa hukumu ambazo hawawezi wakazisoma. Kutafsiri tu kwenyewe lazima walipe pesa. Tunatengeneza mateso na machozi kwa wananchi wengi, muwaonee huruma Watanzania”
habarileo Wednesday, February 3, 2021 6:18:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Kuna wakati magereza yalikuwa na wafungwa zaidi ya 38,000, hivyo naunga mkono rai ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa waheshimiwa majaji na mahakimu kutoa dhamana na adhabu mbadala kila inapostahili. Hii si tu itapunguza rudikano wa wafungwa na mahabusu kwenye magereza bali pia itaipunguzia serikali mzigo wa kuwahudumia wafungwa.”
habarileo Tuesday, February 2, 2021 9:42:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Nimesikia kwamba kamati za maadili za maofisa wa Mahakama wa mikoa na wilaya ambazo kisheria zinaongozwa na Ma-RC na Ma-DC hazikutani, wamepewa madaraka ili kushughulikia masuala ya maadili hawakutani hivyo kushindwa kuchukua hatua kwa watumishi wenye makosa”
habarileo Tuesday, February 2, 2021 9:42:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Wewe hapa Jaji Mkuu umezungumza tena Kiswahili sanifu kweli kizuri kuliko changu cha Kisukuma lakini ukienda kuhukumu kule unaandika Kingereza, hicho Kiswahili unachokitumia hapa kimepotelea wapi. Hii ni challenge (changamoto) kubwa, ni lazima tubadilike, ni lazima tukipende kilicho chetu”
habarileo Tuesday, February 2, 2021 6:34:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Huyu amekuwa mzalendo wa kwanza kuandika kwa lugha ya Kiswahili. Tunamuenzi Baba wa Taifa kwa kuanzisha Mahakama, kwa kuanzisha chuo kikuu, lakini Baba wa Taifa ndiye aliyeanzisha Kiswahili hukumu zenu mnazitoa kwa Kingerezahuyu ni shujaa wa Kiswahili katika Mahakama. Mnajua na ninyi katika Mahakama mpo very rigid (hamtaki kubadilika)”
habarileo Tuesday, February 2, 2021 6:34:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Huyu ameamua, na kwa sababu ameamua kuenzi lugha ya Kiswahili mimi leo ninampandisha cheo kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa”
habarileo Tuesday, February 2, 2021 6:34:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Wewe hapa Jaji Mkuu umezungumza tena Kiswahili sanifu kweli kizuri kuliko changu cha Kisukuma lakini ukienda kuhukumu kule unaandika Kingereza, hicho Kiswahili unachokitumia hapa kimepotelea wapi. Hii ni challenge (changamoto) kubwa, ni lazima tubadilike, ni lazima tukipende kilicho chetu,”
habarileo Monday, February 1, 2021 4:28:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Kahama asilimia 50 ya miradi ya maendeleo inafanywa kwa mapato yao ya ndani na nyie fanyeni kazi, wilaya sio Bahi tu. Halmashauri hii ilikuwa inaliwa sana, Mbunge kasimamie fedha za wananchi nitakuwa nafuatilia, Dodoma na Bahi si mbali nitafuatilia maendeleo,”
habarileo Sunday, January 31, 2021 4:09:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Sheria ya Ardhi Namba 5....hata kama una plot (eneo) lako la makazi na hujaendeleza unanyang’anywa, ila kwa heshima yako mama, naagiza DC na Mkurugenzi wa Halmashauri hii ya Bahi kumpa shamba ekari tatu mama huyu,”
habarileo Sunday, January 31, 2021 1:02:00 PM EAT
Rais Magufuli alisisitiza
:
“Umeanza vizuri hongera sana,moto ulioanza nao endelea nao, usicheke na hawa wakandarasi kamwe, cheka wakati unakunywa maji, halafu zungumzeni na Bodi ya Makandarasi ili kupitia Sheria Namba 17 ya mwaka 1997, wafutwe, wasipate kazi popote Tanzania, kwa vile tuna ushirikiano ndani ya EAC pelekeni majina yao, hatuhitaji watu wa ovyo nchi hii, tunataka ukipewa pesa fanya kazi,”
habarileo Saturday, January 30, 2021 6:34:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Lakini mradi huu ni mkubwa, una uwezo wa kutoa maji lita milioni 9.8 kwa siku sawa na asilimia 213.33 ya mahitaji ya miji hiyo miwili na hivyo kuwa na ziada ya asilimia 113 na tumeamua mradi huu uhudumie pia vijiji vingine 22 vyenye watu 63,000”
habarileo Saturday, January 30, 2021 6:34:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Ni imani yangu kuwa miradi hii na mingine mingi ikikamilika, itatoa huduma kwa wananchi na ninataka miradi hiyo itoe maji sitaki miradi ya kichefuchefu wala hewa”
habarileo Saturday, January 30, 2021 6:34:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Hili nalo tutaliangalia je hawa watumishi wa afya ambao tunaruhusu waajiriwe wanapangwa wapi? Kwa sababu inawezekana tunapanga kuajiri, hawa watumishi wanabaki Dar es Salaam, hawatawanywi kwenye maeneo,”
habarileo Thursday, January 28, 2021 9:11:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Nilijaribu kujiuliza vizuri kama bajeti hiyo imeongezeka kama ilivyoonekana ni sawa na bajeti ya afya nchi nzima ilivyoongezeka kutoka Sh bilioni 31 mwaka 2015 hadi mwaka 2020 ambako ilifikia Sh bilioni 270 sasa inakuaje dawa hazipatikani, kuna mahali kuna tatizo,”
habarileo Thursday, January 28, 2021 9:11:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Tusisubiri mpaka wakati wa uvunaji ufike ndipo muanze kuhangaika kutafuta mahali pa kupeleka magogo, ni lazima tuachane na utaratibu wa sasa wa kuuza nje magogo. Bahati mbaya kwenye magogo nako tunalaliwa sana,”
habarileo Thursday, January 28, 2021 6:04:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Unajifukizia huku unamuomba Mungu unaswali, unasali huku unapiga zoezi la kufanya kazi, la kulima mahindi na kulima viazi, ili ule vizuri ushibe corona ishindwe kuingia,”
habarileo Thursday, January 28, 2021 6:04:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Wenzetu wamefaidika sana na sekta ya mifugo sisi hatujanufaika. Wao wanatengeneza mabegi, mikanda na viatu yenye soko kubwa Ulaya. Nimezungumza na rais na kumuomba kukaribisha wawekezaji lakini pia kuangalia ni namna gani ya kujifunza kwao ili kuendeleza sekta hiyo,”
habarileo Tuesday, January 26, 2021 5:29:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Waasisi wa mataifa yetu Mwalimu Julius Nyerere na hayati Mfalme Haile Sellasie walikuwa mstari wa mbele katika uanzishwaji wa OAU na harakati za ukombozi mwaka 1963. Tumeendelea na ushiano huo mkubwa ulionufaisha nchi zetu katoka nyanja mbalimbali,”
habarileo Tuesday, January 26, 2021 5:29:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Lakini pia Watanzania wamekuwa wakipata fursa ya masomo nchini Ethiopia ambapo jumla ya marubani 75 na wahandisi wa ndege 20 wanasoma Ethiopia,”
habarileo Tuesday, January 26, 2021 5:29:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Uwanja wetu kule Ethiopia tuliochelewa kuujenga kwa sababu hela tulizopeleka kule zililiwa na balozi wetu na kiwanja tukakirudisha kwa kushindwa kutimiza masharti tumemuomba aturudishie na tumemuahidi tutakiendeleza kwa kujenga,”
habarileo Tuesday, January 26, 2021 5:29:00 AM EAT
Rais Magufuli amesisitiza
:
“Wananchi wamechoka na michakato kwa kuwa mradi huo umechelewa kutekelezwa tangu mwaka 1976 mimi wakati huo nikiwa mwanafunzi wa kidato cha pili, hakikisheni utekelezaji wake unaanza haraka na msitishwe na maneno ya watu watakaojitokeza kupinga uwekezaji huu,”
habarileo Tuesday, January 26, 2021 3:08:00 AM EAT
Rais Magufuli amesema
(
about Martha Umbulla
)
:
“Umbulla alikuwa mpole, mchapakazi, na mpenda maendeleo. Nazikumbuka jitihada zake za uongozi akiwa Mkuu wa Wilaya na akiwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,”
habarileo Thursday, January 21, 2021 4:21:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Namshukuru Mungu kuona mradi huu kama utaanza mapema, ninaiamini sana timu yangu ya majadiliano ambayo ina wataalamu wa kutosha, nina imani kubwa ni waaminifu na watiifu kwa taifa lao, madini ya nickel yanatumika kutengenezea vitu mbalimbali vikiwemo vifaa vya kielektroniki, kutengenezea vyuma vigumu, bidhaa za kuzuia kutu na hutumika kwenye injini za ndege,”
habarileo Wednesday, January 20, 2021 7:41:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Na Naibu Waziri ukamweleze Waziri mwezako, na ninyi wabunge mkamweleze Waziri kwamba huu mradi nataka uishe. Huyu mkandarasi kama hawezi kufanya kazi fukuzeni, hakuna kubemelezana hapa, hatukuja kubembelezana, hapa ni kazi tu. Contractor (mkandarasi) usipofanya kazi vizuri unaondokanataka maji”
habarileo Tuesday, January 19, 2021 8:02:00 PM EAT
Rais Magufuli amesema
:
”Kuna shule moja ya msingi Ubungo, Dar Es Salaam inatwa Barango, ina wanafunzi wengi tu. Shule hiyo wanafunzi bado wana kaa chini, madarasa mengine yamebomoka, madawati mengine yamevunjika yameachwa bure. “Mkuu wa Wilaya yupo, Mkuu wa Mkoa yupo, Mkurugenzi wa Ubungo bado anakusanya kodi yupo na Mbunge wa Ubunge yupo tena yupo hapa na ni profesa tena wa Elimu, simama profesa (Kitila Mkumbo) wakuone kwenye jimbo lako, anafundisha elimu, mimi napenda kusema uwazi,” ”Tena wanazungukia maeneo hayo, lakini hiyo shule ya Ubungo Barango, wanakaa chini na wanaona, nina mshukuru huyo mwandishi ameitoa kwenye mitandao, viongozi wa kule wakaanza kusema ni masuala ya kisiasa, hayo sio masuala ya kisiasa hayo ndiyo ninayopenda kuyajua. “Ninazungumza nikiwa Kagera lakini nikienda Dar Es Salaam niyakute hayo madarasa yamekamilika na wanafunzi hawakai chini, nitaenda kuitembelea hiyo shule kama wananisikia wa Dar es Salaam ujumbe umefika”
habarileo Monday, January 18, 2021 2:53:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Rais Dk
)
:
“Niwapongeze kwa sherehe za Mapinduzi ya miaka 57, lakini pia nimpongeze Rais Dk Mwinyi ni kiongozi mzuri hata mapato ya Zanzibar yameanza kupaa. Usiogope kutumbua, tumeanza kuona mwanga wa maendeleo na tunaiona Zanzibar ikiwa kama Dubai,”
habarileo Friday, January 15, 2021 9:54:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Maalim Seif amefanya kazi na baba yake Dk Mwinyi yaani Rais wa Awamu ya Pili (Ali Hassan Mwinyi) na leo anafanya kazi na mtoto wake (Dk Hussein Mwinyi), ana uzoefu mkubwa katika uongozi ninaomba mpe ushirikiano sana,”
habarileo Friday, January 15, 2021 9:54:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Ndio, siasa zilivunja hata ndoa, kisa mmoja Mpemba na mwingine Muunguja sababu za kibaguzi tu, lakini baada ya maridhiano ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa, leo wote ni wamoja na Rais Dk Hussein anaendelea kuvunja ubaguzi huo, Maalim Seif hakikisha unamsaidia rais wako kurudisha mali za Wazanzibari,”
habarileo Friday, January 15, 2021 9:54:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
"Sisi Watanzania na wakazi wa kanda hii tunaona ni zawadi kubwa kwa wewe (Rais Nyusi) kuja kuweka jiwe la msingikwa sababu nimemleta hapa Rais (Filipe Nyusi) kuweka jiwe la msingi, mmejichongea, hospitali lazima ikamilike, hatuwezi kumleta Rais hapa halafu siku nyingine ananipigia simu vipi ile hospitali niseme bado inajengwa hilo sitakubali."
habarileo Tuesday, January 12, 2021 2:46:00 AM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Pia tumeomba tusamehewe deni la kiwanda cha Urafiki dola milioni 15, tumewaomba kwa sababu China ni marafiki wetu na nchi tajiri. Tunajua kwa sheria za China kutoa msamaha ni ngumu lakini tumeoma ili waangalie namna ya kutusaidia,”
mtanzania Sunday, January 10, 2021 9:37:00 AM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Nimeomba watusaidie katika miradi mikubwa mitatu, ule wa Hydroelectricity power wa Njombe Rumakali na Luhuji, nimeomba watujengee barabara kuu ya kilometa 148 kule Zanzibar, lakini pia nimeomba watufutia madeni yetu likiwemo lile tulilolibeba wakati tunajenga reli ya TAZARA la dola milioni 15.7,”
habarileo Friday, January 8, 2021 3:08:00 PM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Watufutie tu kwa sababu nchi ya China ni rafiki yetu na ni nchi tajiri, Mheshimiwa waziri amesema atalifikisha hili ombi,”
habarileo Friday, January 8, 2021 3:08:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Kwa ujumla mazungumzo tuliyoyafanya yalikuwa mazuri na nimemhakikishia Tanzania itaendelea kushirikiana na China kwa sababu ni ndugu zetu, sasa ni wakati wa Tanzania na China kujenga uchumi kwa nguvu zote na kuonesha ushirikiano mkubwa,”
habarileo Friday, January 8, 2021 3:08:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Tumeona vyama vingi havina itikadi hivyo kuanizishwa kwa chuo hichi ni mkombozi kwa wananchi kwani watapata viongozi ambao watakuwa wameandaliwa kwa kuwa na maadili mema,”
habarileo Friday, January 8, 2021 11:15:00 AM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Kuuli siyo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Igunga kuanzia sasahivi,”
mtanzania Monday, December 28, 2020 1:36:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Maelfu ya watu wanaendelea kupoteza maisha kila siku, lakini Tanzania imeepushwa na janga hilo na maisha ya Watanzania yanaendelea kama kawaida,”
habarileo Saturday, December 26, 2020 6:12:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Harold Nsekela
)
:
“Nilimweleza Jaji Harold Nsekela na tulikubaliana kwamba mnaweza kuzipakua fomu kutoka kwenye mtandao, lakini ukishazijaza usizirudishe kwa njia ya mtandao, kila mmoja anajua anarudisha fomu yake wapi kulingana na nafasi yake ya kazi, nafahamu kwa mfano Mheshimiwa Spika huwa analeta kwangu, wewe (Mwangesi) unaleta kwangu, mimi nazileta kwako,”
habarileo Friday, December 25, 2020 1:31:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Nachukua nafasi hii kumpongeza Dk Hussein Mwinyi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa kuapa kuwa Mjumbe wa baraza hili la mawaziri la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nakupongeza sana na karibu kwenye kikao chetu,”
habarileo Thursday, December 17, 2020 9:13:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Haya ndiyo maswali magumu mnayotakiwa kuyafanya, yale mliyoyasoma kwenye nadharia myaweke kwenye vitendo na kuona ni kitu gani kimeshindikana kuwapatia maeneo ya kuchimba madini ya chuma wenye viwanda vya kutengeneza nondo na chuma ili wachimbe, hata kama ni kwa kuwapa bure kwa sababu atatengeneza ajira kwa watu watakaochimba chuma, kwenye sekta ya usafirishaji, ajira viwandani na serikali itakusanya mapato,”
habarileo Saturday, December 12, 2020 10:18:00 AM EAT
Rais Magufuli alisisitiza
:
“Tumesikia Kiwanda Cha Saruji Dangote kule Mtwara, akienda kule anapimiwa, na nimeambiwa kuna mtu amehodhi pale, sifahamu kama keshaondoka au bado yupo? Kwa nini hii coal ya Tanzania isitumike kama nishati mbadala wakati wataalamu wapo? Sasa ni jukumu la ninyi Wizara ya Madini kujipanga. Mfanye kazi vizuri usiku na mchana ili zawadi ya madini mengi tuliyopewa na Mwenyezi Mungu yaanze kutumika,”
habarileo Saturday, December 12, 2020 10:18:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Tumeona tukuweke wewe ukawe kiungo kizuri kwenye wizara hii, wewe ni Profesa lakini haina maana kwamba maprofesa waliowahi kukaa kwenye Wizara ya Madini walifanya vizuri. Kwa hiyo nenda na mtazamo huu, kwa sababu tuliwahi kuwa na waziri na katibu mkuu maprofesa, tena wa madini, lakini mambo hayakwenda vizuri,”
habarileo Saturday, December 12, 2020 10:18:00 AM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Ni vizuri ukafanye uamuzi mbaya kuliko kutokufanya uamuzi, unashindwa kutoa uamuzi kwasababu hutaki uonekane mbaya, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita miradi ya maji zaidi ya 1,400 imekamilika, kwa hiyo mkafanye kazi, kafanyeni uamuzi hasa unaohusu maslahi ya taifa”
mtanzania Thursday, December 10, 2020 1:41:00 PM EAT
Rais Magufuli amesisitiza
:
“Ndani ya Serikali sasa hivi kuna ugonjwa mmoja wa ajabu, kwamba hata mawasiliano yanatumwa kwenye ‘ group za WhatsApp , barua nyingine ni za siri na zinaishia kuvuja. Tuzingatie maadili ya viapo vyetu na tufanye kazi zetu kwa uadilifu mkubwa, Serikali hufanya kazi kwa maandishi”
mtanzania Thursday, December 10, 2020 1:41:00 PM EAT
Rais Magufuli alisisitiza
:
“Nataka wanafunzi wetu wafundishwe historia ya Tanzania na hii itasaidia kujenga uzalendo, vijana hawajui historia ya nchi yetu, inawezekana masomo haya yatasaidia kujua jinsi wageni walivyokuja wakadanganya wazee wetu”
mtanzania Thursday, December 10, 2020 1:41:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Waziri Mkuu
)
:
"Wote nimewaangalia hata wewe uliyeshindwa kuapa na tutateua mtu mwingine ambaye ataweza kuapa vizuri, najua Waziri Mkuu ananiangalia kwa sababu Lindi wametoka yeye na huyu aliyeshindwa kuapa, sasa tutamteua mwingine na wewe tutacheki digrii yako vizuri"
bbc-swahili Thursday, December 10, 2020 7:16:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
"Najua katika kipindi cha miaka mitano mpaka leo, nilitakiwa niwe nimewanyonga watu 256 waliohukumiwa kunyongwa, lakini sijamnyonga hata mmoja,"
habarileo Thursday, December 10, 2020 6:59:00 AM EAT
Rais Magufuli alihoji
:
"Kwa hiyo nimeshindwa kuwaua. Mnisamehe kwa hilo kwa sababu mimi ndio nitakuwa muuaji wa kuuwa wengi kwa sababu wenzangu wameua mtu mmoja au wawili au watatu na wakahukumiwa kunyongwa, halafu mimi niue 256. Si nafuu mimi ninyongwe hapo hapo hata bila kupelekwa mahakamani?,"
habarileo Thursday, December 10, 2020 6:59:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Ndani ya Serikali sasa hivi kuna ugonjwa mmoja, kwa sababu hata mawasiliano yanatumwa kwenye ‘ma-group’ wakati barua zingine ni za siri, mtu anasema tunatakiwa tukutane mahali fulani saa fulani na ajenda yetu ni hii na hii, unakuta labda Makatibu Tawala wa Wilaya wanaandikiana hivyo au Wakuu wa Wilaya au Mawaziri au Makatibu Wakuu na ndiyo maana siri ndani ya serikali zinavuja,”
habarileo Thursday, December 10, 2020 4:45:00 AM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“WAFUNGWA 256 waliohukumiwa kunyongwa wamepunguziwa adhabu na sasa watafungwa Maisha, Sitaki kutenda dhambi,”
habarileo Wednesday, December 9, 2020 3:35:00 PM EAT
Rais Magufuli Alisema
:
"Wote walikuwa wanafaa kupewa uwaziri au unaibu uwaziri. Ilikuwa kazi nzito kufanya uamuzi, Kuna vitu vingi ambavyo tumeviangalia katika uteuzi tuliofanya."
bbc-swahili Wednesday, December 9, 2020 1:21:00 PM EAT
Rais Magufuli anasema
:
“Nitumie fursa hii kulipongeza Bunge la 11 kwa kutoa mchango mkubwa katika kupatikana kwa mafanikio haya,”
habarileo Tuesday, December 8, 2020 8:34:00 AM EAT
Rais Magufuli anasema
:
“Pia serokali itawawezesha wachimbaji wetu wadogo, ikiwa ni pamoja na kuwatengea maeneo ya uchimbaji, kuwapatia mafunzo, mikopo pamoja na vifaa. Na natambua kuwa, wapo baadhi ya watu wamepewa leseni za utafiti na uchimbaji lakini hawajazifanyia kazi; tutazifuta leseni zao, na maeneo hayo kuyagawa kwa wachimbaji wengine, hususan wachimbaji wadogo. Wachimbaji wadogo ni muhimu sana katika kukuza sekta ya madini,”
habarileo Tuesday, December 8, 2020 8:34:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Harold Nsekela
)
:
“Jaji mstaafu Nsekela alikuwa mwadilifu, mzalendo, asiyejikweza na mchapa kazi. Mungu amweke mahali pema Amina,”
mtanzania Monday, December 7, 2020 7:11:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Nchi yetu pia imebarikiwa kuwa na maeneo mengi yanayofaa kwa shughuli za uvuvi, ikiwemo Ukanda wa Pwani, maziwa, mito na mabwawa. Hali hii inafanya sekta hii kuwa na nafasi ya kutoa mchango mkubwa kwenye kukuza Pato la Taifa na pia kupambana na umasikini na tatizo la ajira. Hata hivyo, kwa sasa, mchango wake bado ni mdogo,”
habarileo Tuesday, December 1, 2020 4:55:00 PM EAT
Rais Magufuli alieleza
:
“Hata hivyo, mapato yaliyokuwa yamekusanywa kwa kipindi cha miaka tisa (2009 hadi 2017) yalikuwa shilingi bilioni 29.79, sawa na shilingi bilioni 3.3 kwa mwaka. Kiwango hiki cha mapato hakikubaliki. Hii ndiyo sababu, tunataka, kwenye miaka mitano ijayo, kusimamia vizuri shughuli za uvuvi wa bahari kuu ili Taifa letu linufaike na rasilimali zake, kwa kuhusisha sekta binafsi. Kwa bahati nzuri, tayari, mwaka huu (2020) tumetunga Sheria Mpya ya Kusimamia na Kuendeleza ya Uvuvi wa Bahari Kuu,”
habarileo Tuesday, December 1, 2020 4:55:00 PM EAT
Rais Magufuli alieleza
:
“Tunakusudia pia kujenga bandari kubwa ya uvuvi itakayotoa ajira zipatazo 30,000; na tutaendelea kuihamasisha sekta binafsi kujenga viwanda vya kuchakata samaki,”
habarileo Tuesday, December 1, 2020 4:55:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
"Lengo la serikali ni kuendelea kuboresha elimu inayotolewa ili iweze kutoa maarifa na ujuzi wa kutosha kwa wahitimu, tutahimiza ufundishaji wa masomo ya sayansi na hisabati hususan kwa wanafunzi wa kike”. “Tunakusudia kujenga shule moja ya sekondari kwenye kila mkoa kwa ajili ya kufundisha masomo ya sayansi kwa wasichana,"
habarileo Thursday, November 26, 2020 1:34:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Kwenye miaka mitano ijayo pia, tumejipanga kuendeleza jitihada za kukuza uchumi. Kama unavyofahamu, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, tulijitahidi kusimamia vizuri uchumi wetu, ambapo ulikua kwa wastani wa asilimia saba kwa mwaka,”
habarileo Wednesday, November 18, 2020 11:54:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Aidha, tulifanikiwa kupunguza umasikini wa kipato hadi kufikia asilimia 26.4 kwa takwimu za mwaka 2017/2018. Mafanikio haya, bila shaka, ndiyo yamewezesha, mwezi Julai 2020, nchi yetu kutangazwa kuingia kundi la nchi za uchumi wa kati kutoka kundi la nchi masikini. Na mafanikio hayo yamepatikana miaka mitano kabla ya muda uliopangwa, yaani mwaka 2025,”
habarileo Wednesday, November 18, 2020 11:54:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Na katika hilo, tunalenga kukuza uchumi wetu kwa wastani wa angalau asilimia 8 kwa mwaka na pia kutengeneza ajira mpya zipatazo milioni nane. Tutaendelea pia kuboresha sera zetu za uchumi jumla na sera za fedha na pia kuhakikisha viashiria vyote vya uchumi; ikiwemo thamani ya sarafu yetu, mfumuko wa bei pamoja na viwango vya riba; vinabaki kwenye hali ya utulivu,”
habarileo Wednesday, November 18, 2020 11:54:00 AM EAT
Rais Magufuli amehoji
:
“Na mimi ningeomba wabunge presha mzishushe sababu kazi tuliyoomba hapa ni ubunge wala siyo uwaziri, tulitoka hapa wengine mlikuwa wabunge kwenda kuomba ubunge kwamba tutawatumikia wananchi wetu na tukakabidhiwa ilani ya uchaguzi yenye kurasa 303 sasa mengine yanatoka wapi?,”
mtanzania Monday, November 16, 2020 3:06:00 PM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Hivyo kuna vigezo vingi na kazi ni ngumu kwa hiyo lazima uwe na usawa na umtangulize Mungu ili anayestahili usije ukamuonea. Kwa hiyo ninawaomba tu ndugu zangu mnisamehe tu kwamba inachukua muda mrefu,”
mtanzania Monday, November 16, 2020 3:06:00 PM EAT
Rais Magufuli amesema
(
about Palamagamba Kabudi
)
:
“Kwenye Wizara ya Mambo ya Nje napo hatuwezi tukakosa mtu wa kutusemea tukaendelea kutukanwa watu wanatengeneza majambo yao hawapati majibu kwa sabubu nchi yetu haiwezi kujifungia nikaona Prof. Kabudi naye alimudu nafasi yake nikaona nimrudishe,”
mtanzania Monday, November 16, 2020 3:06:00 PM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Hivyo ni suala ambalo halihitaji haraka, kwa hiyo nawaomba sana wabunge najua maneno ni mengi, kwa kwa waganga nendeni shauli yenu, wengine watawapaka mikosi lakini najua hamuendi,”
mtanzania Monday, November 16, 2020 3:06:00 PM EAT
Rais Magufuli Alisema
:
''Si kwamba hawa wawili ni maarufu sana kuliko waliobaki, miaka ya nyuma niliwateua hawakuwa na majimbo, na niliwaambia waende kwenye majimbo au waende huko walikotoka, wakaenda kwenye majimbo.''
bbc-swahili Monday, November 16, 2020 2:41:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Kwa msingi huo napenda nirudie kupongeza Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kusimamia vizuri uchaguzi mkuu mwaka huu; kuanzia uandikishaji wapigakura, uchukuaji na urejeshaji fomu za wagombea, usimamizi wa kampeni, upigaji kura na utoaji wa matokeo mapema,”
mwananchi Sunday, November 15, 2020 10:49:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Kumekuwepo na vikwazo vingi kwa wawekezaji ikiwemo urasimu mwingi, wawekezaji kuzungushwa na kukatishwa tamaa, nataka mwekezaji mwenye fedha zake akija apate kibali ndani ya siku 14,”
habarileo Saturday, November 14, 2020 11:12:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Na katika hilo, naahidi kushirikiana kwa karibu sana na Rais mpya wa Zanzibar, Mheshimiwa Dk Hussein Mwinyi. Kamwe, hatutakuwa na mzaha na yeyote mwenye kutaka kuhatarisha amani ya nchi yetu; mwenye nia ya kuvuruga umoja na mshikamano wetu; na pia mwenye kutaka kutishia Uhuru wetu, Muungano na Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,”
habarileo Saturday, November 14, 2020 11:12:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Hatutaki mtu yeyote anayetaka kuwekeza asumbuliwe na masuala yasiyo na msingi. Tunahitaji kuwa na mabilionea wengi wa Kitanzania wakiwemo wabunge. Tunataka Watanzania wote washiriki kikamilifu katika kujenga uchumi wa nchi yao,”
habarileo Saturday, November 14, 2020 11:12:00 AM EAT
Rais Magufuli alisisitiza
:
“Namuahidi Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi kwenye miaka mitano ijayo serikali itatoa ushirikiano mkubwa na kufanya kazi kwa karibu na Serikali ya Zanzibar. Tutafanya kazi kwa pamoja kwa lengo la kuleta maendeleo kwa pande zote za Muungano,”
habarileo Saturday, November 14, 2020 11:12:00 AM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Sambamba na hayo, kuhusu nishati, kwenye miaka mitano ijayo, tutaanza utekelezaji wa Miradi ya kielelezo (flagship projects) ya Bomba la Mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga lenye urefu wa kilometa 1,445 pamoja na Mradi wa Kusindika Gesi Asilia (LNG) Mkoani Lindi,”
mtanzania Friday, November 13, 2020 6:34:00 PM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Zaidi ya hapo, tutaendelea kuhamasisha matumizi ya gesi asilia na gesi ya mitungi majumbani, kwenye taasisi, viwanda na magari ili kupunguza uharibifu wa mazingira na athari za mabadiliko ya tabianchi,”
mtanzania Friday, November 13, 2020 6:34:00 PM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Jambo la kwanza na muhimu tutakalolipa kipau mbele kikubwa kwenye miaka mitano ijayo ni kuendelea kulinda na kudumisha tunu za taifa letu yaani amani, umoja na mshikamano, uhuru wa nchi yetu, muungano na mapinduzi matukufu ya Zanzibar. Na katika hilo naahidi kushirikiana kwa karibu sana na Rais mpya wa Zanzibar mheshimiwa Dr. Hussein Mwinyi, kamwe hatutakuwa na mzaha na yoyote mwenye kutaka kuhatarisha amani ya nchi yetu”
deutschewelle-sw Friday, November 13, 2020 2:27:00 PM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Hakuna demokrasia isiyo na mipaka, aidha uhuru na haki vinakwenda sambamba na wajibu na hakuna uhuru au haki isiyokuwa na wajibu. Vyote vinakwenda sambamba. Najua nimeelewaka vizuri. Mheshimiwa spika, kama nilivyoahidi wakati wa kipindi cha kampeini kwenye miaka mitano ijayo tutaendelea kuboresha mazingira ya kufanya biashara kwa wajasiriamali wadogo”
deutschewelle-sw Friday, November 13, 2020 2:27:00 PM EAT
Rais Magufuli aliandika
:
“Kwa niaba ya serikali na Watanzania, nakupongeza Rais Mteule wa Marekani Joe Biden pamoja na Makamu wa Rais, Kamala Harris kutokana na ushindi wenu katika Uchaguzi Mkuu wa Marekani. Nakuhakikishia kuwa Tanzania italinda na kuendeleza uhusiano uliopo baina ya nchi zetu,”
habarileo Thursday, November 12, 2020 11:14:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Hivyo ninaomba waheshimiwa wabunge na Watanzania wote mniombee na mniunge mkono wakati natumbua majipu haya,”
habarileo Thursday, November 12, 2020 9:24:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Kero hizi tutazishughulikia kwa nguvu zetu zote. Wizara, ofisi na taasisi husika zijipange ipasavyo kutatua kero hizi. Nimetaja baadhi ya kero hizi ili nanyi waheshimiwa wabunge mzitambue na mshirikiane na serikali na wadau wengine tuzitatue haraka,”
habarileo Thursday, November 12, 2020 9:24:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Kwa kweli tangu nimefika hapa Tanzania nimeona mambo mazuri na ambayo tunapaswa kuyaiga sisi viongozi wa mataifa mengine,”
habarileo Wednesday, November 11, 2020 9:13:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Katika kipindi chako cha mwanzo ulijitahidi kufanya kazi vizuri, ndio maana tumekupa tena hii nafasi ili ukafanye vizuri zaidi, kikubwa ukamtangulize Mungu katika majukumu yako, maana mimi naamini uwezo unao, Mungu yupo, nina uhakika utafanya makubwa zaidi,”
habarileo Tuesday, November 10, 2020 8:44:00 AM EAT
Rais Magufuli alihoji
:
“Nilitaka nichomekee hapa, kumekuwa na tabia kila serikali mpya au awamu nyingine inapoingia watu wanakuwa na hofu hasa watendaji ndani ya serikali kwamba kunatokea mabadiliko. Sasa wakuu wa mikoa na wilaya wana hofu sana, nawashangaa kwa nini wanakuwa na hofu,”
habarileo Tuesday, November 10, 2020 8:44:00 AM EAT
Rais Magufuli alifafanua
:
“Wanasiasa ambao tumeguswa na hili, mimi rais na makamu wangu, waziri mkuu na mawaziri, mwingine atakayeguswa ni spika na naibu ambao sisi tunapigiwa kura. Sasa mkuu wa mkoa unakuwa na wasiwasi gani ‘unless performance’ yako haikuwa nzuri. Napata meseji kuwa mkuu wa mkoa anasema nimefanya vizuri kwenye kipindi chako,”
habarileo Tuesday, November 10, 2020 8:44:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Kuapisha kunachosha, uanze kuapisha wakuu wa mikoa 26, Ras 26, siwezi. Nitaapisha yule atakayejiondoa mwenyewe. Mchape kazi msiwe na wasiwasi. Tukatatue shida za wananchi”
habarileo Tuesday, November 10, 2020 8:44:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Mwigulu ninamfahamu...na Profesa Mkumbo naye nampenda, ndiyo maana nikasema huyu agombee hapa na yule akagombee Ubungo na nataka wote washinde,”
mwananchi Monday, November 9, 2020 6:43:00 PM EAT
Rais Magufuli amesema
(
about Rais Magufuli
)
:
“Mkuu wa mkoa unakuwa na wasiwasi gani, labda kama utendaji wako haukuwa vizuri, kwa sababu nashangaa napata vimeseji vingine, ‘mheshimiwa, Rais nimejitahidi katika kipindi changu’ kana kwamba nilimwambia kipindi chake kinaisha baada ya mimi kuapishwa,”
mwananchi Monday, November 9, 2020 5:08:00 PM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Mabadiliko yatakayokuwepo ni kwenye mawaziri, kuna ambao watarudi na kuna ambao hawatarudi hili sitaki kusema uongo, nikishamaliza hilo basi wengine wachape kazi tu,”
mwananchi Monday, November 9, 2020 5:08:00 PM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Mkuu wa mkoa unakuwa na wasiwasi gani labda kama ulikuwa ufanyi kazi vizuri kwasababu nashangaa napata vimesji vingine Mhe Rais nimejitahidi katika kipindi changu kana kwamba kipindi chake nilimwambia kinaisha baada ya mimi kuapishwa nimeona hili nilizungumze kwamba Wakuu wa Mikoa,Wakuu wa Wilaya msiwe na wasiwasi”
mtanzania Monday, November 9, 2020 1:24:00 PM EAT
Rais Magufuli Amesema
:
“kwanini nibadilishe Mkuu wa mkoa, kwanini nibadilishe mkuu wa Wilaya, kwanini nibadilishe Mkurugenzi, kwanini nibadilishe DAS Serikali ni ile ile”
mtanzania Monday, November 9, 2020 1:24:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
"Kama tulivyoanza kuchangia kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa kanisa hili, nakuomba sana kama utaniruhusu Askofu na kama sitakukwaza tuchange angalau tuanze kujenga msikiti wa ndugu zetu Waislamu."
habarileo Monday, November 9, 2020 8:01:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Kassim Majaliwa
)
:
“Hata kufanya kazi na mimi ni kazi ngumu, lazima ujipange sawasawa, na hili nawaeleza ukweli kwa sababu na mimi ni mgumu. Hili Majaliwa ameliweza,”
mwananchi Saturday, November 7, 2020 4:02:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Jukumu kubwa na muhimu lililopo mbele yetu hivi sasa ni kuendeleza jitihada za kulijenga na kuleta maendeleo kwa taifa letu. Na katika hilo niwahakikishie Watanzania wenzangu kuwa kiapo nilichokiapa hivi punde na alichoapa Makamu (Samia Suluu Hassan) tutahakikisha tunakienzi kwa nguvu zote,”
habarileo Friday, November 6, 2020 6:26:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Uwepo wenu hapa na salama mlizotutumia, sio tu zinatupa nguvu za kuwatumikia wananchi vizuri, bali ni ishara ya uhusiano na ushirikiano uliopo kati yetu. Napenda niwahahakishie kama ilivyokuwa kwenye miaka mitano iliyopita, kwenye miaka mitano ijayo tutaendeleza na kukuza zaidi uhusiano na ushirikiano kati yetu pamoja na taasisi mnazoziwakilisha,”
habarileo Friday, November 6, 2020 6:26:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Hii ni ishara nyingine kuwa Mungu analipenda taifa letu la Tanzania, tangu tumepata Uhuru mwaka 1961, nchi imepita kwenye mitihani mingi na Mungu ametuvusha salama...Tumshukuru sana Mungu kwa maajabu anayolifanyia taifa hili,”
habarileo Friday, November 6, 2020 6:26:00 AM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Hata njaa kali ilipoingia nchini mwetu, Tanzania walitupatia mahindi, hata Uganda nao walituletea mahindi, ndio viongozi wazalendo kabisa katika ukanda wetu,”
habarileo Thursday, November 5, 2020 4:13:00 PM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Uchaguzi umekwisha, uchaguzi umekwisha, uchaguzi umekwisha. "Uchaguzi sasa umekwisha, jukumu kubwa lililopo mbele yetu ni kuendeleza jitihada za kujenga na kuleta maendeleo kwa Taifa letu na niwahakikishie kuwa kiapo nilichoapa na alichoapa makamu wangu (Samia Suluhu Hassan), tutahakikisha tunakienzi kwa nguvu zote,”
habarileo Thursday, November 5, 2020 2:28:00 PM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Sambamba na hilo tutatekeleza kwa namna kubwa katika kukuza uchumi na kushughulikia changamoto za umasikini zinazowakabili Watanzania. Ukosefu wa ajira kwa vijana na kero mbalimbali kwa wananchi,”
habarileo Thursday, November 5, 2020 2:28:00 PM EAT
Rais Magufuli alieleza
:
“Gharama ya umeme wetu ipo juu na uwezo wetu wa kuzalisha kwa sasa ni megawati 1,600, mradi huu wa megawati 2,115 ukikamilika tutausambaza umeme nchi nzima na tutaushusha bei kwa sababu huwezi kujenga uchumi wa viwanda kama huna umeme wa uhakika na wa gharama nafuu, mpaka sasa viwanda vipya 8,470 vimeanzishwa maeneo mbali mbali hapa nchini,”
habarileo Thursday, November 5, 2020 9:04:00 AM EAT
Rais Magufuli alieleza
(
about Tanzania Bara
)
:
“Mwaka 2012, Benki ya Dunia ilisema Tanzania itaweza kufikisha umeme kwenye vijiji vyote 12,280 ifikapo mwaka 2100, mimi nasema tutapeleka umeme kwenye vijiji vyote ndani ya miaka mitano ijayo,”
habarileo Thursday, November 5, 2020 9:04:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Baba wa Taifa alikuwa haongozwi ongozwi wala kupelekeshwapelekeswa. Tukasema haiwezekani Watanzania ambao chakula chao chenyewe wanakitafuta kila siku, leo ufungiwe nyumbani,”
habarileo Thursday, November 5, 2020 7:32:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Tutaimarisha masoko kwenye maeneo yenye shughuli za uchimbaji madini na kuhamasisha ujenzi wa viwanda vya uchenjuaji madini,”
habarileo Thursday, November 5, 2020 5:14:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Nitaimarisha pia Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kiwe na uwezo wa kutoa wataalamu mbalimbali wa anga. Lakini pia nitaongeza matumizi ya intaneti kutoka asilimia 43 ya sasa hadi kufikia asilimia 80,”
habarileo Thursday, November 5, 2020 5:14:00 AM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Serikali nitakayoiunda itakuwa ya uwazi, uwajibikaji na usawa bila kubagua mtu kwa rangi au eneo analotoka ambayo itakayokuwa ikizingatia nidhamu kwa watumishi, itakayokuwa na kasi kwa kuimarisha huduma za kijamii.”
habarileo Monday, November 2, 2020 3:48:00 PM EAT
Rais Magufuli amesema
(
about Rais Magufuli
)
:
“Nasimama mbele yenu kwa mara ya kwanza nikiwa Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. Nimekula kiapo kuwa Rais wa nane wa Zanzibar,”
habarileo Monday, November 2, 2020 3:48:00 PM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Mmetupa ushindi mkubwa sana ambao umetuachia deni kubwa sana, ninamuomba Mungu anisaidie katika kipindi hiki cha pili tuweze kukidhi haja za Watanzania,”
mwananchi Sunday, November 1, 2020 1:58:00 PM EAT
Rais Magufuli aliongeza
:
“zimebakia siku moja ili Watanzania mkapige kura kwa kuamua mazuri, hivyo ni vizuri kuitumia siku hiyo katika kujenga umoja wa watanzania”
habarileo Tuesday, October 27, 2020 2:23:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Waziri Mkuu
)
:
“Ndani ya mwezi mmoja muwe tayari kutatua tatizo hilo, kama hakuna fedha kama ambavyo meneja amesema zungumza na Waziri wa Fedha au Katibu Mkuu ili kushughulikia suala hilo,”
habarileo Monday, October 26, 2020 7:28:00 PM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Nilienda Rwanda nilialikwa na Rais Paul Kagame, akaenda kunitembeza kwenye jumba la makumbusho ya mauji ya Kimbari. Nilienda kujifunza umuhimu wa kutunza amani, yaani niliona mafuvu ya vichwa vya watu maelfu mpaka Watoto. Ukiona unachanganyikiwa,”
habarileo Sunday, October 25, 2020 8:22:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Na huu ni ukweli na siwezi kuuficha, na hili liwe fundisho kwetu sisi Watanzania na vizazi vinavyokuja baadaye, kwamba kubinafsisha ndege, treni na meli ni dhambi kubwa,”
habarileo Sunday, October 25, 2020 6:51:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Lakini pia hivi karibuni mtaanza ujenzi wa reli ya Katavi kwenda Bandari ya Kalema ili kurahisisha usafiri kati yetu na nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC),”
habarileo Sunday, October 25, 2020 6:51:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Nimesikitishwa na vifo vya watanzania wenzetu waliopoteza maisha katika ajali hii, nawapa pole wafiwa wote na nawaomba wawe na moyo wa uvumilivu na ustahimilivu katika kipindi kigumu cha majozi,”
habarileo Sunday, October 25, 2020 6:51:00 PM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Niwahimize Watanzania wenzangu tupende vya kwetu na nitashangaa sana kama vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vitaendelea kuagiza viatu kutoka nje nitashngaa sana wanafunzi waendelee kuvaa viatu vya nje,”
mwananchi Thursday, October 22, 2020 4:40:00 PM EAT
Rais Magufuli alieleza
:
“Nilitamani kufika mikoa yote ya Tanzania, lakini niwaombe Watanzania mtambue kuwa mimi ni binadamu nisingeweza kufika kila mahali, lakini pia pamoja na kufanya kampeni, nina majukumu pia ya kutekeleza ya kitaifa, ndiyo maana nimewatuma wasaidizi wangu,”
habarileo Friday, October 16, 2020 2:31:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Jakaya Kikwete
)
:
“Nikamuuliza Mzee Kikwete, akasema mimi Msoga. Nikaogopa kumuuliza mzee Mwinyi kwa sababu alikuwa na miaka 90 na kitu, nikaona nikimuuliza halafu likatokea la kutokea nitaonekana nimeleta uchuro. Lakini mimi kwa dhamira yangu, nikasema nitazikwa Chato,”
mwananchi Friday, October 16, 2020 12:11:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Angeweza kuzikwa Lushoto au eneo jingine lolote, lakini ndani ya dhamira yake alitaka azike kijijini kwake. Tujifunze kwa upendo mkubwa aliouonyesha kwa wananchi wake,”
mwananchi Friday, October 16, 2020 12:11:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Waheshimiwa wabunge, naamini nitakuwa sijakosea nikisema kazi kubwa imefanyika kwenye sekta ya elimu,”
mwananchi Friday, October 16, 2020 12:11:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
"Kama wiki hii tunayoianza kesho hali itaendelea hivi, nimepanga kufungua vyuo ili. wanafunzi wetu waendelee kusoma na pili nimepanga pia sisi kama taifa kuruhusu. michezo iendelee kwa sababu michezo ni sehemu moja ya burudani kwa Watanzania,"
mwananchi Friday, October 16, 2020 12:11:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Leo nahitimisha kampeni zangu katika Mkoa wa Dar es Salaam hapa Kawe, nawashukuru sana wananchi wa Dar es Salaam kwa kuniunga mkono, nina deni kubwa kwenu, asanteni sana Dar es Salaam kwa mapenzi makubwa mliyoyaonesha kwangu,”
habarileo Thursday, October 15, 2020 2:08:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Kawe mmechelewa sana, mwaka 2015 niliwaomba mumchague Kippi Warioba, lakini mlinyima kura, kwa hiyo sasa naomba msirudie makosa, fanyeni mabadiliko ya kweli kwa kumtoa aliyekuwepo nileteeni Askofu Gwajima,”
habarileo Thursday, October 15, 2020 2:08:00 PM EAT
Rais Magufuli alieleza
:
“Nilitamani kufika mikoa yote ya Tanzania, lakini niwaombe Watanzania mtambue kuwa mimi ni binadamu nisingeweza kufika kila mahali, lakini pia pamoja na kufanya kampeni, nina majukumu pia ya kutekeleza ya kitaifa, ndiyo maana nimewatuma wasaidizi wangu,”
habarileo Thursday, October 15, 2020 2:08:00 PM EAT
Rais Magufuli aliongeza
(
about Tanzania Bara
)
:
“Tanzania ina Mungu kwa sababu anatusikia. Na katika kipindi cha corona uchumi wetu ulizidi kupaa hata kutangazwa kuwa nchi ya uchumi wa kati. Hongereni watanzania kwa kushikamana,”
habarileo Wednesday, October 14, 2020 1:37:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
"Tangu nianze kampeni sijawahi kuhudhuria mkutano ambao wananchi wanakubali kunyeshewa mvua kwa kunisubiri mimi, ni upendo wa mkubwa sana, mmeniachia deni kubwa katika maisha yangu, upendo huu lazima tuulipe mara 100 kwa wananchi wa Ubungo na Kibamba,"
habarileo Tuesday, October 13, 2020 6:05:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Mmesikia wenyewe aliyekuwa Meya ya Ilala kwa chama cha upinzani, kabla ya kukihama hicho chama, Omary Kumbilamoto amekiri na kutubu hapa kwamba vikao vya madiwani yaani baraza la madiwani lilikuwa ni la upinzani tupu na amekiri hapa walihujumu miradi yote ya maendeleo isitekelezwe Ilala kwa madai kuwa wakitekeleza watailetea sifa serikali. Sasa ametubu, tumuombe Mungu amsamehe, lakini iwe fundisho kwenu msirudie tena kuwapa kura upinzani, kazi yao ni kupinga maendeleo,”
habarileo Tuesday, October 13, 2020 1:22:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Serikali imefanya mengi kwa Jiji la Dar es Salaam, Ilala ikiwemo, tuna mradi wa DMDP ambao umetengewa shilingi bilioni 660 kuboresha barabara za jiji hilo na za Ilala zipo; tunaomba mtuchague ili tukamalizie zile ambazo bado hazijajengwa,”
habarileo Tuesday, October 13, 2020 1:22:00 PM EAT
Rais Magufuli aliwaambia
:
“Aidha, tumepanga kukamilisha awamu ya pili ya mradi wa mabasi ya mwendokasi kutoka Kariakoo hadi Mbagala, kwa hiyo wananchi wa Mbagala wataanza kufaidi mabasi ya mwendokasi, pamoja na Daraja la Selander na Daraja la Juu la Gerezani. Tukamilisha pia miradi ya kimkakati ya upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam na ujenzi wa reli ya kisasa ya Dar es Salaam hadi Dodoma,”
habarileo Saturday, October 10, 2020 11:30:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Hii ndiyo Dar es Salaam mpya tunayotaka kuijenga, wakati tunaomba madaraka mwaka 2015 tuliwaaambia tunataka kuibadilisha Dar es Salaam, tutajenga barabara za juu, hakuna aliyeamini, niliwaambia jamani mimi mtani wenu nataka niwatengenezee Dar es Salaam, bado hamkuamini, leo ninyi watani zangu na wana-Dar es Salaam ni mashahidi kwamba Dar es Salaam tunaibadilisha,”
habarileo Saturday, October 10, 2020 11:30:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Dar es Salaam ni jiji kuu la biashara hapa nchini, linachangia mapato mengi ya serikali na kutoa mchango mkubwa katika Pato la Taifa. Katika miaka mitano iliyopita, Dar es Salaam imeongoza kwa mapato ya serikali yatokanayo na kodi, asilimia 90 ya mapato ya kodi yanatoka Dar es Salaam, pia ni jiji lenye watu wengi wanaofikia milioni sita na mwaka 2030 watakuwa milioni kumi hivyo kuwa miongoni mwa majiji manne makubwa Afrika likiwemo Jiji la Lagos, Luanda na Kinshasa,”
habarileo Saturday, October 10, 2020 11:30:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Umuhimu wa bandari hizi kwa Malawi ni mkubwa, Malawi tunaunga mkono uboreshaji huu ambao utakuwa na manufaa ya moja kwa moja kwetu,”
habarileo Friday, October 9, 2020 12:00:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Huu mradi nimeambiwa tangu ulipoanza uko chini ya mkandarasi kutoka Kampuni ya Heinan Construction Limited, ulitakiwa kumalizika mwezi wa saba, haujamalizika, naomba niseme kwa dhati kisingizio eti ni corona,”
habarileo Friday, October 9, 2020 11:13:00 AM EAT
Rais Magufuli aliongeza
:
“Kwa sababu jamani naomba niongee ukweli, sijafurahishwa kabisa na kasi ya ujenzi wa mradi huu, mkataba huu ni wa shilingi bilioni 71, kuanzia mwezi wa saba hadi hiyo Januari ni miezi minne, hii si haki. Palitakiwa watu wawe wanafanyakazi hapa wanaingiza pesa,”
habarileo Friday, October 9, 2020 11:13:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Lazarus Chakwera
)
:
“Waziri, huyo mkandarasi aanze kukatwa fedha za kuchelewesha huu mradi. Tukienda kwa utaratibu huu miradi mingi itachelewa. Nazungumza mbele ya Baba Askofu mstaafu Lazarus Chakware, haiwezekani. Mkandarasi na mradi ni mzuri lakini hatuwezi kuvumilia uzembe huu,”
habarileo Friday, October 9, 2020 11:13:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Ifike mahali tutambue kuwa hakuna mtu atakayetutengenezea uchumi wetu, sisi ndio wa kuzijenga nchi zetu, sisi ndio wa kuleta mabadiliko, hatuna kaka wala dada, sisi viongozi ndio wa kuleta mabadiliko ya kiuchumi ya nchi zetu na njia pekee ni kushirikiana kwa pamoja kwa kumshirikisha Mungu,”
habarileo Friday, October 9, 2020 11:13:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Naomba walimu mlipuuze hilo tangazo, ni la kipumbavu, serikali inajali sana walimu wote hata wa ngazi ya cheti. Mke wangu ni mwalimu wa cheti, mke wa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ni mwalimu wa cheti,”
habarileo Tuesday, October 6, 2020 9:35:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Ninawapongeza walimu wenzangu wa madaraja yote kwa kuadhimisha Siku ya Walimu Duniani, serikali inatambua mchango wenu ni mkubwa kwa taifa na itaendelea kuboresha maslahi na mazingira yenu ya kazi, endeleeni kuchapa kazi. Tulianza pamoja, tutamaliza pamoja,”
habarileo Tuesday, October 6, 2020 9:35:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Nawapenda sana walimu na ndio maana nilioa mwalimu,”
habarileo Tuesday, October 6, 2020 9:35:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Rais Zanzibar
)
:
“Ili mambo haya yote yaweze kutekelezwa, naomba mnipe kura nyingi za urais, pia mpeni kura za kutosha Dk Mwinyi, Mwinyi ni chaguo sahihi kuiongoza Zanzibar kwa kipindi hiki, namfahamu ni kijana makini, mwadilifu, mchapakazi, hapendi uzembe na anachukia rushwa, namwamini Mwinyi atayasimamia haya kwa maslahi ya Wazanzibari,”
habarileo Sunday, October 4, 2020 8:54:00 AM EAT
Rais Magufuli amesema
(
about Rais Magufuli
)
:
“Zanzibar inahitaji maadili na kama wanahitaji mtu wa Kariba hiyo Mwinyi ni mtu sahihi, na ninakuomba ukipata urais hakikisha makamu wako wa pili wa Rais atokee Pemba”
habarileo Saturday, October 3, 2020 5:25:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Rais Magufuli
)
:
“Leo tumesimama kuomboleza kifo cha kijana yule, alipondwa kichwa chake, na waliokuwa wanamponda ni vijana wenzake, WatanzaniaBaba wa Taifa ameliacha hili Taifa likiwa salama, mimi kama Rais nisingependa niliache Taifa hili likiwa na hali ya ugomvi namna hii,”
habarileo Friday, October 2, 2020 9:46:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about David Silinde
)
:
“Nawaomba wana Tunduma mniletee Silinde, halafu mje mniulize maji, na nimeshaanza kuifanya hii miradi hii, tutayatoa maji Ileje,”
habarileo Friday, October 2, 2020 9:46:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Ndiyo maana nimekuja Tunduma kuwaomba kura, lakini pia nimekuja kuwaonya, na hili mimi nawaambia kwa dhati bila kupepesa, haiwezi ikawa inafikia wakati wa kura tu hizi za siasa, zitugawanye watu kiasi hiki, Tanzania haijafikia mahali hapo, angalieni nchi ambazo hazina amani, mna ushahidi wa kutosha, kuna nchi mpaka leo zinapigana, Tanzania pamekuwa mahali pa salama pa kimbilio la kila mtu, hatuko tayari kuichafua Tanzania kwa kuanzia Tunduma,”
habarileo Friday, October 2, 2020 9:46:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Naamini viongozi wa Serikali ya Mkoa na wizara mnanisikia, kampeni ya makomandoo ni marufuku kuanzia leo, kwa hiyo akina mama bebeni tu ujauzito vizuri ili tuongeze idadi, idadi ya watu inapokuwa kubwa na uchumi nao unakua kama nchi za wenzetu za China na India,”
habarileo Friday, October 2, 2020 6:39:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Serikali ya CCM ni ya vitendo siyo ahadi, mniamini na mtuamini, tunayoahidi tutayatekeleza, nasema ahadi za kweli,”
habarileo Friday, October 2, 2020 6:39:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Lakini nawaomba akina mama kuanzia sasa muanze kwenda kliniki kwa hiyari kwa sababu serikali tunatumia fedha nyingi kujenga vituo vya afya na hospitali kwa gharama kubwa kwa ajili yenu ili kuokoa maisha ya mama na mtoto”
habarileo Friday, October 2, 2020 6:39:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Pia tumejenga vihenge sita vyenye uwezo wa kuhifadhi tani 20,000 za mazao kwa gharama ya Sh bilioni 11.4, na hivyo kuongeza uwezo wa kuhifadhi mazao kutoka tani 17,000 hadi tani 37,000, ujenzi wa vihenge hivi utapunguza upotevu wa mazao,”
habarileo Friday, October 2, 2020 6:39:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Nina mapenzi ya dhati na Mbeya, ninataka kuifanya iwe lango kuu la utalii na uchumi katika ukanda huu wa Nyanda za Juu Kusini, huduma za jamii ikiwemo afya, elimu tutaziboresha miaka mitano ijayo, nataka iwe hivyo na ndivyo Ilani yetu ya CCM inavyosema,”
habarileo Thursday, October 1, 2020 8:57:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Tunataka tuimarishe huduma za kijamii za afya hapa, ili tunaposema tunaibadilisha Mbeya kuwa lango kuu la uchumi na utalii, pia huduma za jamii za tiba za kibingwa zitolewe hapa na tupate wateja kutoka nchi jirani,”
habarileo Thursday, October 1, 2020 8:57:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Tutafanya hayo yote ndani ya miaka mitano ijayo, tunataka kuibadilisha Mbeya, ndege kubwa zitue hapa muda wote, lakini kufanikiwa kwa haya kutategemea na ninyi,”
habarileo Thursday, October 1, 2020 8:57:00 AM EAT
Rais Magufuli alisisitiza
(
about Joseph Mbilinyi
)
:
“Ndio maana nawaomba nileteeni Dk Tulia, nishauriane naye pia jinsi ya kugawa Mbeya iwe na wilaya mbili kama yalivyo majiji mengine mfano Dar es Salaam na Mwanzahata Sugu (mbunge anayemaliza muda wake Joseph Mbilinyi) naye namuomba anipe kura, huu sio wakati wa kubishana, ni wakati wa maendeleo na maendeleo hayana chama,”
habarileo Thursday, October 1, 2020 8:57:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Fedha zipo hapa hapa za kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo, zamani zilikaliwa na mafisadi, tumewabana sasa zinakwenda kuhudumia wananchi,”
habarileo Wednesday, September 30, 2020 7:22:00 AM EAT
Rais Magufuli alieleza
:
“Tunataka uchumi wa Watanzania, tunataka mabilionea Watanzania,”
habarileo Tuesday, September 29, 2020 9:10:00 AM EAT
Rais Magufuli alieleza
:
“Mfano miaka mitano ijayo tutakuza uchumi kwa wastani usiopungua asilimia nane. Miaka mitano iliyopita tumetoka kwenye uchumi wa kutupwa hadi tumeingia kwenye uchumi wa kati,”
habarileo Tuesday, September 29, 2020 9:10:00 AM EAT
Rais Magufuli alifafanua
:
“Tumejenga vituo vya afya 487, ajira zilipatikana kwa waliokuwa wanajenga, wanaopeleka saruji, misumari, kokoto, lakini pia tulinunua ndege 11 hii nayo ni ajira kwani marubani zaidi ya 500 waliajiriwa. Tumejenga barabara zaidi ya kilometa 3,000 makandarasi zaidi ya 8,500 waliajiri watu, hizo zote ni ajira,”
habarileo Tuesday, September 29, 2020 9:10:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Oktoba 28, mwaka huu asubuhi na mapema nendeni mkawafagie nje ili wajifunze, Watanzania sio wa kufanyiwa majaribio. Kwanza, wanadai kuweka nchi kwenye mfumo wa utawala wa majimbo, halafu wanaeleza pia kwenye ilani yao kuweka madini yetu rehani (dhamana), sasa mwisho wataweka wanyama wetu, ni kuingiza nchi kwenye utumwa mwingine,”
habarileo Wednesday, September 23, 2020 8:55:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Meneja Tanroads kaeni na wenzako, chagueni barabara za mjini hapa zitakazojengwa kwa lami urefu wa kilometa kumi, pesa itakuja,”
habarileo Wednesday, September 23, 2020 8:55:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Tusipokuwa na amani suala la utulivu uliopo litaondoka, hatutaweza kwenda mashambani kulima, hatutaenda kanisani au msikitini, kwa ujumla maisha yatakuwa magumu sana hata masuala ya ujenzi wa viwanda haitawezekanawaulizeni wakimbizi waliopo hapa ambao wengine wameshakuwa Watanzania walikimbia amani kwao, tusifanye makosa, tutajuta,”
habarileo Tuesday, September 22, 2020 10:36:00 AM EAT
Rais Magufuli alisisitiza
(
about Mwalimu Nyerere
)
:
“Mwalimu Nyerere alituweka pamoja makabila yetu zaidi ya 120, hakutaka mfumo wa majimbo ya ukanda kwa sababu kufanya hivyo ni kutekeleza matakwa ya wanaotaka kuja kututawala na kupora rasilimali zetu baada ya sisi kuingia mtegoni na nchi kuchafuka, hayo mambo ndio wanafundishwa huku nje, tusikubali kuifarakanisha nchi kamwe,”
habarileo Tuesday, September 22, 2020 10:36:00 AM EAT
Rais Magufuli alisisitiza
:
“Hivi tungekubali mfumo huo, je, leo fedha za ujenzi wa barabara za kuunganisha Kigoma na mikoa mingine shilingi bilioni 567 zingetoka wapi? Tabora tumeleta maji kutoka Ziwa Victoria kwa gharama ya shilingi bilioni 600, je, Tabora wangezitoa wapi? Maana hazikutolewa na maeneo hayo tu, bali ni michango ya nchi nzima, kataeni mbinu za kutugawa, zikataeni kwa nguvu zote”
habarileo Tuesday, September 22, 2020 10:36:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Hili gonjwa corona ni la ajabu sana sisi hapa tumepambana na cha ajabu tumebanana tu, ila niwashukuru Watanzania kwa kuungana nami kuomba kwa Mungu, maana mlinisikia, tukamuomba Mungu akasikia akatuponya, maana kama tungefunga nchi na watu hali ingekuwa mbaya,”
habarileo Tuesday, September 22, 2020 10:36:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Vitambulisho havilazimishwi, mfanyabiashara halazimishwi kuwa nacho, ni suala la hiari kwa wale wanaovitaka wapewe. Mkuu wa mkoa wa hapa toeni elimu kuwa ukiwa nacho unafanya biashara popote Tanzania kwa mwaka mzima, haya ndiyo maagizo yangu,”
habarileo Tuesday, September 22, 2020 10:36:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Hatuwezi tukapeleka kwa miaka mitano vijiji 17 tu, tulitakiwa tuwe tumepeleka kwenye vijiji 61 vibaki 17 tu, hii ni kero lazima nibebe mimi mwenyewe,”
mtanzania Monday, September 21, 2020 5:04:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Nataka siku moja nikija kuweka jiwe la msingi niikute lami mpaka Uvinza, natoa maagizo Jafo uwaletee bilioni tano kuanzia Jumatatu ziwe zimeshafika Uvinza,”
mtanzania Monday, September 21, 2020 5:04:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Mazungumzo yetu yamekuwa mazuri sana, tumetoa maagizo tume ya kudumu ya mawaziri ianze kukutana kujadili masuala ambayo yako ‘pending’,”
mtanzania Monday, September 21, 2020 5:04:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Tunataka tutengeneze ‘hub’ ya hapa Kigoma ili tuwasaidie wananchi wa Burundi waweze kufanya biashara na wenzao wa Tanzania, tumeiweka ‘centre’ ya biashara ambayo itaunganisha Burundi, Rwanda na DRC, hata bandari tutaipanua ili kubeba mizigo ya kutosha,”
mtanzania Monday, September 21, 2020 5:04:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Wataalam wa wizara zinazohusika wakae na kujadili, tunakaribisha wafanyabiashara wa Burundi walete dhahabu yao wauze, huu ni wakati wa kujenga uchumi wa nchi zetu hizi mbili,”
mtanzania Monday, September 21, 2020 5:04:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Joyce Ndalichako
)
:
“Sasa ukiangalia vijiji vingi vimefikiwa na umeme lakini hapa Uvinza ndani ya miaka mitano sasa ni vijiji 17 tu vyenye nishati hiyo, bado vijiji 61, hii niseme wazi haijanifurahisha, ni kero, na Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako uko hapa, kamweleze Waziri Nishati sijafurahishwa,”
habarileo Monday, September 21, 2020 10:59:00 AM EAT
Rais Magufuli alieleza
:
“Madini ya nickel yanapatikana eneo la Msangati Burundi na sisi kule Kabanga, tumekubaliana tukiunganisha nguvu zetu tutangeneza kiwanda cha kuchenjua madini hayo na kupata faida kubwa zaidi,”
habarileo Sunday, September 20, 2020 8:20:00 AM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Kituo chetu cha Uwekezaji kimesajili miradi 16 kutoka Burundi yenye thamani ya dola milioni 26.42 ambazo zimetoa ajira zaidi kwa watu 544 na kuna taarifa zaidi ya kampuni kumi kutoka Tanzania nazo zimewekeza Burundi,”
habarileo Sunday, September 20, 2020 3:57:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Kituo chetu cha Uwekezaji kimesajili miradi 16 kutoka Burundi yenye thamani ya dola milioni 26.42 ambazo zimetoa ajira zaidi kwa watu 544 na kuna taarifa zaidi ya kampuni kumi kutoka Tanzania nazo zimewekeza Burundi,”
habarileo Sunday, September 20, 2020 3:57:00 AM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Kujenga mtambo wa pamoja wa kuchenjua madini ya Nicol, Tanzania tunayo Kabanga na wao wanayo. Mazungumzo yamekwishaanza ili tuuze na kupata ajira na fedha,”
habarileo Sunday, September 20, 2020 3:57:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Nawaambia ukweli jipangeni kwa ajili ya kutajirika, limeni, fanyeni biashara ili muuze, mabasi na magari mengine yatapita hapa kwenda mikoa mingine na nchi hizo mtauza, hakuna atakayekuja kuwapa pesa za bure, jipangeni kwa ajili ya kutajirika, tena nyie bahati nzuri ni wachapakazi, mlikosa miundombinu ya barabara ninawaletea na umeme pia,”
habarileo Friday, September 18, 2020 9:35:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Ndio maana nasema mnichagulie Mbunge Nditiye(Atashasta), ili iwe rahisi kwangu kumbana na kumwagiza atekeleze changamoto hizo zote zilizobakia, urais au ubunge sio kuangalia sura, changueni maendeleo na mkoa huu mnabahati mmepata mawaziri watatu,”
habarileo Friday, September 18, 2020 9:35:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Msifanye makosa hapa Kasulu, Kigoma ilisahaulika, ni mkoa ulioachwa nyuma kwa miaka mingi, nikasema lazima niweke mikakati mikubwa ya kufufua uchumi, nikajiuliza nani atafanya mambo ya Kigoma, nikampa Waziri wa Fedha, Dk Philip Mpango mtu wa Kigoma, nikatafuta wa elimu ili ashughulikie na Kigoma, nikamleta Profesa Joyce Ndalichako ni wa hapa Kasulu, barabara nikamleta Atashasta Nditiye,”
habarileo Friday, September 18, 2020 9:35:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“nimekuja hapa kwa ukumbusho mkubwa, hapa ndipo mahali nilipewa warranty (hati) ya kusafiria kwenda kusoma Mkwawa High Schoolnimepanga baada ya kustaafu nitakaa Kagera na ndio maana nina ng’ombe wangu huku, ninapapenda, na watu wa Kagera ni wazuri wanahitaji maendeleo na uchumi,”
habarileo Thursday, September 17, 2020 10:11:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Ninapapenda Kagera, hata nilipokuwa natafuta Katibu wa chama niliangalia wee nchi nzima, nikamuona Dk Bashiru ataweza, ametoka maisha ya chini, amefanya biashara ya ndizi pale Kemondo, ni mzalendo kati ya wachache wa kufuata miiko ya Mwalimu Julius Nyerere, ndio maana nikamteua awe Katibu Mkuu wa CCM,”
habarileo Thursday, September 17, 2020 10:11:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Wale wote wanaodai fedha za kahawa vyama vya ushirika nalichukua hilo, serikali tutalipa yote, nimemuagiza Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa na Waziri wa Kilimo wanapanga njia bora ya kuzilipa, CCM haiwezi kuwa serikali ya kudhulumu wananchi,”
habarileo Thursday, September 17, 2020 10:11:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Nataka mniamini, ahadi ninazozitaja ziko ndani ya Ilani ya CCM ya mwaka 2020-25, sio kama baadhi ya vyama vya siasa ambavyo wanatoa ahadi zao kichwani, hawana ilani, nikiahidi, ninatekeleza, na mfano nzuri ni Ilani ya mwaka 2015, tumetekeleza ahadi nyingi,”
habarileo Thursday, September 17, 2020 10:11:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Nataka mtu akitoka hapa aende Kemondo, wafanyabiashara wafanye biashara zao kwa uhuru, waende Musoma, Kisumu (Kenya), Uganda kisha warudi Bukoba ili mzunguko wa pesa uwe mkubwa, watu watengeneze maisha yao,”
habarileo Thursday, September 17, 2020 10:11:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Nafahamu mkuu wa shule anashikiliwa na Polisi, ninaomba wakati wanaendelea na uchunguzi, huyo mkuu wa shule wamuachie pia, ila wadhibiti na kujua kama ni ajali ya kweli au kuna uzembe, kwa sababu hata akiwa nje ya mahabusu atashirikiana na polisi kutoa taarifa, naomba huyo baba nina hakika hana moyo mbaya wa kuchoma watoto wetu, ningeomba awe nje, akiendelea kukaa ndani tunamuongezea mateso, aliwalea kama watoto wake,”
habarileo Thursday, September 17, 2020 9:22:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Tusichague kwa jazba, na kuangalia viongozi wapenda maneno, tukikosea, tutajuta maana hakuna maendeleo mtakayoyaona,”
habarileo Wednesday, September 16, 2020 8:17:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Naombeni mnipe miaka mitano tu, tutafanya makubwa katika muda huo, nikimaliza miaka yangu mitano hiyo, sitaki niongezewe hata siku moja, wapo wengine ndani ya CCM wanaoweza pia kuongoza, nataka nipumzike na mimi niangalie wengine wanavyofanya kazi,”
habarileo Wednesday, September 16, 2020 8:17:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Ninafahamu hapa kuna maneno maneno, chama ndio kinachagua nani anafaa kwa wakati gani, sasa masuala ya nani kapitishwa yalishaisha, tuliamua tuwachague hao tuliowapitisha kwa sababu ndio wanaofaa kuongoza kwa muda huu, na pia uongozi ni kupeana nafasi unaweza kuongoza leo kesho akaongoza mwingine,”
habarileo Wednesday, September 16, 2020 8:17:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Tunataka Kemondo, hapa bandarini pawe salama wafanyabiashara wafanye biashara zao kwa uhuru na tija, tumeamua kuanzia sasa tozo kwa tani moja ya mazao au bidhaa zitozwe shilingi 27, 000 badala ya ile ya awali ya hadi shilingi 130,000,”
habarileo Wednesday, September 16, 2020 8:17:00 AM EAT
Rais Magufuli anasema
:
“Hii ndiyo maana tuliamua kutumia makusanyo tunayoyapata kufanya uwekezaji wa kutosha katika huduma za afya,”
habarileo Tuesday, September 15, 2020 7:41:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Afrika Mashariki
)
:
“Na ndiyo maana leo tumesaini maana yake sasa pameisha. Maana yake ujenzi wa bomba la mafuta la Afrika Mashariki litakalojengwa kutoka Hoima Uganda hadi Tanga lenye jumla ya kilometa 1,445 unaanza,”
habarileo Monday, September 14, 2020 6:25:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Afrika Mashariki
)
:
“Huu mradi umeshughulikiwa kwa muda mrefu, nampongeza Mzee Museveni amefanya mambo yasiyowezekana. Afrika Mashariki tuwe na mafuta? Tumekuwa tukisikia mafuta yapo Uarabuni sijui wapi lakini Museveni ameyatafuta tena kwa kutumia watu wa Uganda,”
habarileo Monday, September 14, 2020 6:25:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Tunaomba kura za kutosha ili tukafanye mengine makubwa zaidi, tunataka tukayalinde mafanikio tuliyoyapata, tukasimamie miradi inayoendelea kutekelezwa na tukaanzishe miradi mipya kwa sababu uwezo wa kufanya haya tunao,”
habarileo Saturday, September 12, 2020 1:00:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Hii yote ni kuifanya Tanzania waione kwamba ni nchi kweli imeingia uchumi wa kati, kama tumekuta nchi inahesabika uchumi wa chini leo uchumi wa kati…ndiyo wakati wa kutupa kura ili tufike uchumi wa juu na mbinu za kufika huko tunazo,”
mtanzania Friday, September 11, 2020 11:28:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Kuongoza ni kutoa lengo ndicho tunachokifanya kwa maendeleo mapana ya nchi yetu, mimi bado naamini tuna mambo mengi ya kufanya katika nchi hii na hasa kuibadilisha,”
mtanzania Friday, September 11, 2020 11:28:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Kwenye madini tutaimarisha udhibiti na usimamizi wa uchimbaji madini ili uweze kunufaisha taifa, tutawezesha wachimbaji wadogo wafanye shughuli zao kwa tija. Tutaimarisha masoko kwenye maeneo yenye shughuli za uchimbaji madini na kuhamasisha ujenzi wa viwanda vya uchenjuaji madini,”
mtanzania Friday, September 11, 2020 11:28:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Sekta hii inakua kwa kasi na imeajiri vijana wengi, tutaimarisha usimamizi wa hati miliki ili wasanii wanufaike na kazi zao. Sekta ya sanaa na michezo tutaibeba kwa nguvu kubwa zaidi,”
mtanzania Friday, September 11, 2020 11:28:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Ninajua wako baadhi ya watu wanaweza wasiamini kwamba tunaweza kuyatekeleza, naomba Watanzania watuaminia uwezo wa kuyatekeleza tunao kama ambavyo tumeweza kuyatekeleza yale mengine kwa kipindi cha miaka mitano,”
mtanzania Friday, September 11, 2020 11:28:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Tutatengeneza wilaya ambayo itakuwa ya mfano katika nchi hii, hapa pameshakuwa mji mkubwa hivyo tunataka kuleta mabadiliko ya kweli katika mji wenu,”
mtanzania Friday, September 11, 2020 11:28:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Chama Cha
)
:
“Nawaomba sana kura zenu mkipigie Chama Cha Mapinduzi ili haya niliyoyaeleza tuweze kuyatekeleza kwa kasi,”
mtanzania Friday, September 11, 2020 11:28:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Tunaomba kura za kutosha ili tukafanye mengine makubwa zaidi, tunataka tukayalinde mafanikio tuliyoyapata, tukasimamie miradi inayoendelea kutekelezwa na tukaanzishe miradi mipya kwa sababu uwezo wa kufanya haya tunao, na nia ya kuyafanya tunayo, kilichobaki ni kura kutoka kwenu Watanzania,”
habarileo Friday, September 11, 2020 12:34:00 AM EAT
Rais Magufuli alieleza
:
“Hii ndiyo mipango ya maendeleo tunayoitengeneza na Tanzania ninayotaka kuijenga, haya ndiyo tunayopanga sisi kama taifa, na huu ndiyo wakati wa kutupatia CCM kura nyingi ili tukafanye kazi na kuiingiza nchi kwenye uchumi mkubwa zaidi kwa sababu mbinu za kutafuta fedha tunazo na mbinu za kuwabana mafisadi tunazo,”
habarileo Friday, September 11, 2020 12:34:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Hii ni mara ya kwanza kwa Tanzania kufanya Uchaguzi Mkuu kwa kutumia gharama zetu wenyewe bila kutegemea wafadhili. Hakuna hata senti tano ya wafadhili au fedha kutoka nje, huku ndiko kujitawala na kujitegemea,”
habarileo Thursday, September 10, 2020 12:12:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Unapotaka kujenga taifa lolote, haya ni mambo ya msingi kuanza nayo, kwa hiyo tumejipanga kwa miaka mingine mitano kuleta mabadiliko kweli kwa nchi yetu, nawathibitishia Watanzania, yote tunayoahidi na tusiyoyaahidi tutayatimiza kwa spidi kubwa, mnipime kwa miaka 10, nawahakikishia tutafanya maajabu,”
habarileo Tuesday, September 8, 2020 7:55:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Uliniambia maneno mazuri ‘kwamba mama yako anaumwa na kuteseka kwa makusudi ya Mungu ili wengine tupone’. Leo unaniombea kura. Asante sana mama. Mungu akujalie sana katika maisha yako hasa katika kukienzi chama cha mume wako,”
habarileo Sunday, September 6, 2020 11:22:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Rais Magufuli
)
:
“Mshaurini nitampa kazi serikalini ni mtoto wetu tunampenda wala hatuna tatizo, na mimi ndugu zangu sina tatizo na mtu yeyote, kwani kazi lazima uwe rais? Mwache Rais Magufuli sisi tutakupa kikazi utakachoweza kufanya kwa sababu sisi wote ni wamoja, akija mwambieni Magufuli atakupa kazi kwanini uhangaikie hii kazi ambayo hutashinda?”
mtanzania Wednesday, September 2, 2020 12:22:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Tunataka watoto wasome bure, ndio maana siku zote nilikuwa nasema zaeni, hakuna kuzaa kwa mpango, matiti ya kunyonyesha watoto tunayo, maziwa tunayo na wanaume wapo, wakina mama wapo na shule wanasoma bure, Serikali ipo,”
mtanzania Wednesday, September 2, 2020 12:22:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Kwa nini turudi nyuma tulikotoka? Na ndio maana tunasema katika miaka mitano ijayo, tutatoa elimu bure, ndio maana tunaomba ndugu zangu mturudishe,”
mtanzania Wednesday, September 2, 2020 12:22:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Kweli leo mmefunga kaziimedhihirisha wazi kwamba hapa ni makao makuu,”
habarileo Sunday, August 30, 2020 10:16:00 PM EAT
Rais Magufuli alisisitiza
:
"Tupeni tena miaka mitano tukawafanyie makubwa zaidi Watanzania, mambo mazuri na makubwa yanakuja, tuendelee kuwa wamoja,"
habarileo Sunday, August 30, 2020 10:16:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Mtakumbuka, zamani, kabla ya utaratibu huo kuanza, wajasiliamali wadogo walikuwa wakibugudhiwa sana na mgambo, ikiwemo kunyang’anywa mali zao. Hivyo, kwa kuanzisha utaratibu wa kutoa vitambulisho hivyo, tumedhihirisha kuwa Serikali ya Awamu ya Tano ipo kwa ajili ya wanyonge,”
habarileo Saturday, August 29, 2020 9:41:00 PM EAT
Rais Magufuli amesema
:
“Mahali ambapo ni Makao Makuu ni lazima pazungukwe na watu wanaomtukuza Mungu, Baba Askofu kama utaniruhusu na hili nakuomba sana, basi tutumie siku ya leo pia tuchange tuanze kujenga Msikiti wa ndugu zetu Waislamu ambao Msikiti wao ni mdogo na wapo pale kwa ajili ya kumtukuza Mungu na baadhi ya wasaidizi wangu ni Waislamu na yupo anaitwa Alhaji na ameshaenda kuhiji,”
habarileo Sunday, August 23, 2020 5:58:00 PM EAT
Rais Magufuli anasema
:
“Niwapongeze wasanii mmeitangaza Tanzania kwa maslahi mapana, Serikali iko pamoja nanyi kuhakikisha inatetea maslahi yenu, najua mmeteseka sana nahitaji mtoke huko COSOTA na kuingia kwenye Wizara ya Habari ili kazi zenu zionekene na mfaidike ”
habarileo Thursday, August 20, 2020 5:45:00 PM EAT
Rais Magufuli alihoji
:
“Kazi ya Meneja wa Tanroads Mkoa ni pamoja na kuitunza barabara hii, nitashangaa kama ataendelea kuwepo mpaka kesho au keshokutwa, lakini hata Waziri wa Ujenzi, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Mtendaji Mkuu wa Tanroads, hamuwezi hata kupitia barabara zenu?,”
habarileo Friday, July 31, 2020 12:59:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Nilipata fursa ya kuongea na mzee Mkapa kwa simu akiwa hospitalini saa chache kabla hajafariki, nakumbuka aliniambia John usiwe na wasiwasi naendelea vizuri, sikujua kwamba maneno yale yalikuwa ya kuniaga, kazi ameikamilisha. Namshukuru Mungu kwa zawadi ya Mkapa,”
mtanzania Wednesday, July 29, 2020 3:45:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Jakaya Kikwete
)
:
“Saa nyingine machozi yanakuja tu, msinishangae sana, hata mzee Kikwete (Jakaya Kikwete) nilimuona juzi anadondosha machozi, tena Kikwete ni Kanali lakini alitoa chozi, kwa hiyo msinishangae mimi,”
mtanzania Wednesday, July 29, 2020 3:45:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Mzee Mkapa alimwibua Dk. Hussein Ali Mwinyi ambaye kwa sasa ni mgombea urais Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), aliyekuwa mwandishi wake wa hotuba Balozi Ombeni Sefue, baadaye aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu Kiongozi,”
mtanzania Wednesday, July 29, 2020 3:45:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Benjamin Mkapa
)
:
“Kama ambavyo nimekuwa nikisema mara nyingi bila Mzee Mkapa mimi nisingekuwa hapa nilipo, itoshe tu kusema Mzee Mkapa ni shujaa wangu na ni mtu muhimu sana katika historia ya maisha yangu,”
habarileo Wednesday, July 29, 2020 6:21:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Saa nyingine machozi huwa yanakuja, hata Kikwete nilimuona analia, na Kikwete ni Kanali lakini naye aliyatoa machozi kwa hiyo msishangae shangae. Unajua kifo saa nyingine huwezi ukakivumilia, lakini niseme kweli Mzee Mkapa alinilea kama mtoto wake na alikuwa akinionesha upendo mkubwa sana,”
habarileo Wednesday, July 29, 2020 6:21:00 AM EAT
Rais Magufuli alieleza
(
about Benjamin Mkapa
)
:
“Kwa hakika sisi Watanzania hatuna budi kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa Mzee Mkapa kuwa kiongozi wetukifo cha Mzee Mkapa ni ukumbusho kwetu sote kuacha alama hapa duniani,”
habarileo Wednesday, July 29, 2020 6:21:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Benjamin Mkapa
)
:
“Mzee Mkapa alikuwa kiongozi mahiri, shupavu, jasiri, mchapakazi, muadilifu, mchamungu, mfuatiliaji, mwenye msimamo usiyoyumbishwa, mzalendo kwa taifa lake, mwanadiplomasia nguli na pia mpenda amani, umoja na mshikamano,”
habarileo Wednesday, July 29, 2020 6:21:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
"Ni ukweli usiopingika kwamba nchi yetu, Afrika na dunia imeondokewa na mtu muhimu sana,"
deutschewelle-sw Tuesday, July 28, 2020 1:29:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Rais Magufuli
)
:
"Kutokana na mchango mkubwa katika maisha yake binafsi kwa taifa kwa ujumla, Rais Mkapa ataendelea kuwa shujaaa wake daima,"
deutschewelle-sw Tuesday, July 28, 2020 1:29:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Rais Magufuli
)
:
“Kupitia kwako Rais, tunatoa salamu zetu za pole kwa familia, ndugu, marafiki na jamaa wote wa marehemu,”
habarileo Saturday, July 25, 2020 2:31:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Jengo la Intelijensia atazindua Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa ambaye pia amezindua la Takukuru Ruangwa. Jengo la Mpwapwa atazindua Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, jengo la Manyoni atazindua Spika Job Ndugai, jengo la wilaya ya Masasi atazindua Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru John Mbungo, jengo la Namtumbo atazindua Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), George Mkuchika”
habarileo Thursday, July 23, 2020 9:30:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Ilipojitokeza fursa tukamteua kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, sasa sifahamu unajua vijana saa nyingine hawaridhiki haraka haraka, hasa waliozaliwa miaka ya 1982, lakini ni matumaini yangu atakwenda kuitumikia kazi yake vizuri,”
mtanzania Sunday, July 19, 2020 5:22:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Waliochukua fomu kuomba kuwania kwenye majimbo wapo 6,533, Viti Maalum 1,539, uwakilishi 133 jumla 8205, bado leo na kesho(ijumaa),”
habarileo Thursday, July 16, 2020 8:35:00 PM EAT
Rais Magufuli amesema
:
"Hii kazi umeipata kwa sababu Mungu alitaka, mkamtangulize Mungu katika kazi zenu lakini pia mkawatumikie wananchi maskini katika maeneo yenu, nipende kusisitiza kwamba katika kazi hizi, kuridhika ni jambo muhimu sana, unajua vijana saa nyingine hawaridhiki harakaharaka haswa waliozaliwa miaka ya 1982"
habarileo Thursday, July 16, 2020 8:35:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
(
about Ali Kiba
)
:
“Ukiona Ali Kiba anakaa pamoja na Diamond hapo ndio unaiona nguvu ya CCM au ukimuona Harmonize aliyemkimbia Diamond leo anamsifia hadharani hapa inapendeza kweli, hii ndio Tanzania tunayoitaka, mimi shabiki yenu nawafuatilia sana,”
mtanzania Monday, July 13, 2020 12:12:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Sanaa imesota sana huko, nawaahidi wasanii kabla ya kufika Jumapili inayofuata haya yote nitayamaliza, Waziri Mwakyembe nataka kabla haujaenda kuchukua fomu kule kwenu uje uchukue barua nitakayokuwa nimeisaini ya kuhamisha shughuli za COSOTA kutoka kwenye Wizara ya Viwanda na Biashara kuja kwenye Wizara yako ili hawa vijana wafaidike na usanii wao,”
mtanzania Monday, July 13, 2020 12:12:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Tafuteni mwanajeshi yeyote mumuulize, ametulia hakugombana na wanajeshi alisimamia usalama wa nchi hii. Kwa hiyo nitamshangaa mtu anayeweza kusi- mama akasema hatoshi. Alisimamia mizinga leo asitoshe kusimamia Zanzibar?,”
habarileo Sunday, July 12, 2020 7:39:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Sijui sasa mtasema niko na nani,”
mtanzania Saturday, July 11, 2020 1:25:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Nimemwagiza Katibu Mkuu amwalike kesho (leo) Kinana na viongozi wetu wastaafu, CCM kinapenda viongozi wanyenyekevu na hakuna malaika,”
mtanzania Saturday, July 11, 2020 11:53:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Yule mwingine sina sababu ya kumtaja ameishajiondoa moja kwa moja,”
mtanzania Saturday, July 11, 2020 11:53:00 AM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Tumebakiza vijiji 3,156 tu. Tukichaguliwa hatuwezi kushindwa vijiji hivi vitatu tu,”
habarileo Thursday, July 9, 2020 2:26:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Haijawahi kutokea. Kiwango cha juu kabisa tulichowahi kukusanya kwa mwezi ilikuwa ni sh bilioni 43,”
habarileo Wednesday, July 8, 2020 2:25:00 PM EAT
Rais Magufuli alisema
:
“Jana (juzi) nilikuona Kaimu Kamishna Jenerali wa dawa za kulevya ukienda kwenye milima na watu wa Clouds, kila mahali mlipopita mlikamata magunia ya bangi, hii inatia shaka kwa viongozi wanaoniwakilisha kule, haiwezekani mpaka wewe utoke Dodoma Makao Makuu ndiyo ukazione bangi wakati kule viongozi wapo,”
habarileo Tuesday, July 7, 2020 1:30:00 PM EAT